-Malkia Elizabeth alimtuza kahaba huyo nchini New Zealand kwa juhudi zake kupigania biashara ya ngono kuhalalishwa
-Hayo yalitokana na ukahaba kuorodheshwa kuwa uhalifu nchini humo
- Catherine Haealy hakuamini kuwa angepata tuzo hiyo
Tukio la kihistoria lijishuhudiwa jijini Wellington nchini New Zealand pale Malkia Elizabeth alipomtuza kahaba Catherine Haealy, 62, kwa juhudi zake za kupigania ukahaba kuwa biashara huru.
Malkia Elizabeth alitoa tuzo hiyo kwa Haealy Jumatatu, Juni 4 katika sherehe ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa nchini humo.
Tuma neno ‘NEWS’ kwa 40227 ili kupata habari muhimu pindi zinapochipuka
Kahaba huyo alituzwa kutokana na juhudi zake za kushinikiza mabadiliko kwenye sheria za New Zealand mwaka wa 2003 nchini humo ili kuwawezesha makahaba kufanya biashara zao kihalali.
![](https://cdn.statically.io/img/cdn.tuko.co.ke/images/1120/0fgjhs3r5u4tlu48bg.jpeg)
Habari Nyingine: Mvulana wa miaka 10 ashangaza Wakenya kwa kipaji chake cha utangazaji (video)
Haealy alisema kuwa hakuwahi kufikiria kuwa angewahi kushinda tuzo kama hiyo.
“Sikutarajia tuzo kubwa kama hii. Ningali katika mshangao. Ni heshima kubwa sana kwangu.” Catherine Haealy alisema.
Habari Nyingine: Mwanamke aandika CV kwenye mtandao kutafuta mchumba
Catherine alikiri kuwa juhudi zake zilimpa wasiwasi sana kutokana na hali ilivyokuwa, akifichua akiishi kwa woga kuwa angekamatwa.
“Kwa kweli, nilidhani ningekamatwa, wala sio kupata tuzo kubwa kama hii. Nilizidiwa na hisia. Niguswa sana.” Haealy alinukuliwa na jarida za Telegraph kuyasema hayo.
Habari Nyingine: Mkewe Alfred Mutua amtambulisha dadake mrembo kwa umma
Kahaba huyo aliripotiwa kuchangia katika kupitishwa kwa sheria iliyotaja ukahaba kama biashara huru katika nchi tofauti.
Mwanamke huyo alianza juhudi za kupigania ukahaba kutambuliwa kama biashara huru kuanzia mwaka wa 1989.
Habari Nyingine: Mastaa wa soka Ujerumani wapewa marufuku ya kutofanya ngono, kombe la dunia muhimu
Haki alizokuwa akipigania zilijumuisha kutambuliwa kwa haki za makahaba, kutobaguliwa kutokana na kazi zao na kupata malipo mazuri kwa huduma wanazotoa kwa wateja wao.
New Zealand hutoa tuzo kama hizo mara mbili kwa mwaka, mwanzo wa mwaka na kwenye maadhimisho ya siku ya kuzaliwa ya Malkia Elizabeth II mbazo hufanyika mapema mwezi Juni.
Waziri mkuu wa zamani wa New Zealand Bill English pia allituzwa kuwa ‘knight’, tuzo inayotolewa kwa wanajeshi na viongozi walioleta mafanikio fulani kwa nchi.
Una taarifa motomoto au sakata ambayo ungependa tuichapishe? Wasiliana nasi kwa news@tuko.co.ke, mwangi.muraguri@tuko.co.ke , kwenye WhatsApp: 0732482690 na kwenye Telegram: Tuko News
Nimeshiriki mapenzi na zaidi ya wanaume 100, nimewahi kujaribu kujiuwa mara 5 | TUKO TV
Subscribe to watch new videosChanzo: TUKO.co.ke
ncG1vNJzZmijmajEorTIpaBnrKWgvG%2BvzmeinmdibIJ6gZhmpJqkm56ubrHLorGampWptW6tzK2ss5ldoK6prcGaZJqkma6ysbXGmqWimV2drqy1jLOYZpqZlsCprdGaZLKZXaO0sLrOZ5%2BtpZw%3D